Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Urembo ulionishinda mimi.....

Kuna vingine sijawahi kujaribu, vingine nimejaribu vikanizidi uwezo....

1: kupaka wanja kwenye nyusi
Huu urembo ulinishinda tangu enzi za mwalimu, kila nikijaribu naona nakua Kama nyau hasa hasa wanja mweusi, basi nikijaribu kupaka nafuta naendelea na mambo mengine, mara chache nimejaribu wanja wa brown napaka kwa mbaaali naona unakuja kuja mdogo mdogo ntaweza.

2: kuvaa wig/kushonea weaving
Hapa nimeinua mikono, wig nilivaa mwaka flani wakati naanza kusokota dread siwezi kwenda kazini vile, nikanunua wig kwanza dukani tu naambiwa linauzwa elf 25 nikashtuka nlijua buku ten, nikanunua nikavaa mmh najiona nakua kama kanjibai, linawasha, lina joto nlipata shida, nywele zilivorefuka sijarudia tena huu urembo siuwezi kabisa.

3: kubandika kucha
Nilijaribu siku moja kutoa ushamba, naona shost angu kila siku anabandika anapendeza, akanipeleka namie nikabandika mmh siku hiyo hata kutandika kitanda nilishindwa, kuchomeka shuka kwenye godoro ikawa tabu, siku chache nikazoea, siku ya kuzibandua sasa yani zinang'olewa utadhani nimetekwa nlikua na kazi ya kupiga kelele kama kimbwa, sirudii tena sitarudia kabisa.

4: kubandika kope
Hii kujaribu tu siwezi make, nikiwaona kina mwajuma ndalandefu wanavokua huwa nacheka, kope zinasimama utadhani mtu kavaa kofia, yana wenyewe haya

5: kupaka cream/kujichubua
Hii kazi ya kujipa mateso hii, uso mweupe miguu myeusi, kuna siku nliwekewa maji ya cream bila kujua ushamba huu, nimeulizwa tu niweke maji nkajibu eeh weka nlijua labda glycerin, duh siku mbili tu nkaanza kuwa kama tumbili....

Wewe huwezi nini?

Nb: naombeni mniambie mafuta ya nywele natural, naona nywele zinakatika

paka mafuta ya Kuza kwenye nywele.

Post a Comment

0 Comments