Header Ads Widget

Responsive Advertisement

MASWALI NA MAJIBU KUHUSU MAPENZI (PART 01)



Mke wangu kaolewa na rafiki yangu. Nifanyeje?
Mke wangu wa miaka mitatu ambaye tumezaa pamoja watoto wawili ameniacha akaolewa na mwanamume rafiki yangu wa kufa kuzikana. Sasa siwezi kumwamini mtu yeyote anayedai kuwa rafiki. Nishauri

= Kuna watu kama hao ambao hujifanya marafiki kumbe ni mbwa-mwitu. Yaliyokupata ni sehemu ya maisha na pia funzo kwako kwani sasa umejua kuwa sio kila mtu anayekuita rafiki ambaye anakutakia mema.
**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********




NIKIMPIGIA SIMU HACHUKUI
NINA mpenzi ambaye nampenda sana lakini nikimpigia simu hachukui. Nifanye nini?



= Una hakika huyo ni mpenzi wako ama ni kuota tu unaota naye? Angekuwa mpenzi wako hangekataa kuchukua simu. Na iwapo kweli ni mpenzi wako, labda umemkosea ama ameamua kukuacha. Chunguza ujue ukweli.



**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********


MCHUMBA ALIPACHIKWA MIMBA NA MWENGINE
KUNA msichana ambaye tumekuwa wapenzi kwa miaka miwili sasa na tulikuwa tumepanga kuoana. Lakini alipachikwa mimba na mwanamume mwingine na akajifungua. Nitafanya nini ili nimuoe?



= Hali kwamba huyo unayemuita mpenzi wako alikubali kuzaa na mwanamume mwingine ni ishara kamili kuwa hakuthamini. Mbona unang’ang’ania kumuoa?


**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********







NILIMTEMA MUME WA MIAKA MINNE KWA KUNITESA

NILIKUWA nimeolewa kwa miaka minne na nikapata mtoto. Nilimpenda sana mume wangu lakini alikuwa akinitesa kwa kunipiga na kushikana na wanawake wengine bila kunificha. Tumetengana kwa mwaka mmoja na sasa anataka turudiane. Lakini nimepata mwingine anayenipenda. Nishauri.



= Kama usemayo ni ya kweli, huko ulikotoka ni sawa na jehanamu na usitamani kurudi. Kama umepata mwanamume mwingine anayekupenda na unampenda shukuru Mungu na uendelee na maisha yako.

**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********





JE, ANANIPENDA AU ANANIDANGANYA?
KWAKO shangazi. Kuna kijana fulani ninayempenda sana naye anasema ananipenda. Ajabu ni kuwa huwa hanipigii simu hadi wakati anaponihitaji. Je, ananipenda ama ananihadaa tu?



= Mawasiliano ya ni kimojawapo cha viungo vya kuongezea penzi ladha na ni ajabu kwamba mwenzio huwasiliana nawe pale tu anapokuhitaji. Jihadhari na kijana huyo asije akawa anakutumia tu na akichoka nawe akuteme.



NINAPOENDA LAKINI ANA MTOTO AMBAYE SI WANGU
Kuna mrembo tunayependana sana na anataka nimuoe ilhali ana mtoto ambaye si wangu. Nifanyeje?



= Mtoto hafai kuwa kikwazo palipo na penzi la dhati. Kama unampenda msichana huyo na una uwezo wa kumtunza yeye na mtoto, basi muoe.

**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********




BAADA YA UHUSIANO WA MIAKA MINNE BADO NAMSUBIRI
NINA umri wa miaka 26 na kuna msichana ambaye tumekuwa na uhusiano kwa miaka minne sasa. Nataka kumuoa lakini ananiambia nisubiri kwa miaka miwili. Ningojee ama niachane naye?



= Kama mmekuwa pamoja kwa miaka minne sielewi ni kwa nini unaona vigumu kusubiri miaka miwili tu kama kweli unampenda na unataka awe mke wako.

**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********



NIKIMTUMIA UJUMBE, ANANIELEZA ANA MKE
 Kuna mwanamume ambaye tumekuwa wapenzi kwa miaka mitatu. Majuzi aliniambia anataka mtoto na nikakubali kwa sababu nampenda sana. Sasa nina mimba yake na hataki hata kujibu simu zangu. Nikimtumia SMS ananiambia ameoa. Nifanye nini?



= Ulikosea kwa kukubali kupata mimba na mwanamume huyo kabla hajakuoa rasmi. Sijajua alikuwa na nia gani kwako lakini ukweli ni kuwa amekutwika mzigo kisha akakuhepa. Iwapo unajua mimba ni yake, subiri ujifungue kisha umshtaki kortini ili alazimishwe kugharamia malezi ya mtoto wake.


**********       ******    ************         *****            **********       *******       ********




UFICHUZI WAKE WANISHTUA
Kuna msichana ambaye tumekuwa na uhusiano kwa miezi mitatu sasa na huniambia ananipenda. Majuzi nilishtuka aliponiambia kuna kijana waliyependana miaka mitatu iliyopita na ameshindwa kumuacha. Nishauri.



= Huenda alikubali ombi lako katika juhudi za kumsahau mpenzi wake huyo wa zamani lakini ameshindwa. Muulize msimamo wake hasa kuhusu kijana huyo usije ukapoteza wakati wako kwake na hatimaye warudiane.

Post a Comment

0 Comments