Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Nakujuza vitu 9 muhimu unahitaji kuwa navyo kwenye chumba chako cha kulala

1. A COMFORTABLE RUG/ ZULIA
You need a rug /zulia inategemea unapenda la manyoya sana au la kawaida tu wengine wanapenda liwe chumba kizima wengine nusu tu ,either way ni wewe upendavyo tu. Zulia linaweza kuwa ndogo au kubwa wewe tu unavyopendezwa. Zile rugs zenye manyoya sanaa make sure unakuwa msafi usimwage mwage vitu vyenye maji maji maana yakiingiaga maji harufu yake utalichukia.




2. UWE NA MUONEKANO AU MANDHARI WA CHUMBA CHAKO
Wengi wanafikiri themes za bedroom ni kwa watoto peke ake la hasha hata kwa wakubwa pia,kuna wanaopenda romantic themes,all white etc.
Hapa naona huyu alipenda kuwe pa brownish flani hivi




3. MITO MINGI AU MICHACHE KADIRI UTAKAVYOPENDA
Hizi throw pillow ni a must have kwenye bedroom yako, kuna hapo za kurembea na za kulalia you need enough of them, ila kuna wengine wanapenda mingi inakuwa half of the bed ni mito tu,another day ntakuja waonyesha jinsi ya kuipanga.



4. SEHEMU YA KUKAA AU KUPUMZIKA AMBAYO SIO KITANDANI
Kitandani ni mahali pa kulala japo kuna wengine mwakaa ila tafuta kitu cha kukalia kama sofa kama hizo hapo juu au viti.

Wengine wanatumia ile space ya dirisha kujenga hapo droos kwa ajili ya kuhifadhia vitu na juu unaweka cushions na mito panatosha kukaa tena kuna view nzuri kama uko gorofani unaka hapo kusoma kitabu au kufikiria tu na kupanga mipango yako. viti pia vyapendeza





5. COLLECTION YA VITU UNAVYOVIPENDA
Ni vizuri kuwa na collection ya vitu vyako unavyopenda kuvitumia kama decor mfano vitabu mbalimbali
Kama una awards zako au decor zozote zile waweza tengenezea shelf kama hilo unaweka .




6. DROO AU VIKABATI VIDOGO VYA CHUMBANI
Umuhimu wa kuwa na a night stand mbali tu na kuwa ni decor pia waweza hifadhi vitu humo kama books,remotes ,taa ,weka hata maji ya kunywa kama huwa wanywa usiku.
Unaweza pia kwenye night stand ukaweka picha za familia yako au ya kwako ,flowers etc.





7. PICHA ILA SIO ZA WATU
Last week nliwaletea wall decor huko tulisema weka picha za familia ila huku chumbani weka tu za urembo au kitu kinacho ku Inspire zaidi. picha za flowers au wanyama pia





8. GODORO IMARA/QUALITY MATTRESS
Make sure una invest kwenye matress yenye quality nzuri.Utalala comfortable





9. ELEMENTS OF DRAMA
Chumba kidogo kiwe na drama mfano hizo bold colors kama hiyo red au hiyo picha nzurii ya lips

Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Post a Comment

0 Comments