Header Ads Widget

Responsive Advertisement

HISTORIA YA VALENTINE DAY:



Siku ya wapendanao ni sikukuu ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 14 Februari ya kila mwaka (Valentine Day).

Historia yake imeanzia karne ya 3 huko Roma ambapo alikuwapo padri Valentinus ambaye akaja kuheshimiwa kama mtakatifu hasa tarehe hiyo.
Hadithi zilizosababisha sikukuu kuenea

Inasemekana kwamba Kaisari wakati huo alikuwa Claudius II: yeye aliona kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule asiyeoa wala kuwa na familia (kapera). Hivyo alipiga marufuku ndoa kwa askari.

Valentinus alipinga jambo hili hivyo kuendelea kufungisha ndoa kwa siri. Mfalme Claudius alipopata habari hizi aliamuru Valentinus akamatwe na kuuawa.

Kuna hadithi nyingine ya kuwa akiwa gerezani Valentinus aliandika barua ambayo ilikuwa na salamu za kwanza za Valentine kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani; mwisho wa barua alihitimisha kwa maneno haya: Kutoka kwa Valentinus wako.

Toka hapo Valentine anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na sikukuu yake kuadhimishwa kote duniani.

AU

Siku ya Valentines Day asili yake ni kutoka Dola ya Warumi. Ni siku ya kumbukumbu (memoria day) na sehemu nyingine ni (festum) maana yake siku kuu ya daraja la kwanza kwa kumkumbuka Padre Valentine aliyeuawa na utawala wa kirumi sababu ya kutetea waumini wake kufunga ndoa badala ya kuishi na vimada tu. Lakini sikukuu hiyo imeenea sana katika nchi za magharibi na baadaye karibu sehemu kubwa ya ulimwengu kuisherehekea kama siku yamapenzi kinyume cha dhamira ya Mt. Valentine.

Watawala wa dola ya kirumi walikuwa na fikra za kueneza dola ya kirumi duniani kote na hivyo vijana hawakutakiwa kuoa, ili wawe huru muda wote kwenda vitani kupigania nchi. Wakioa hawangekuwa na uhuru wa kwenda vitani bali kuwa na famiia zao. Vijana wengi wakawa na mtindo wa kuwa na vimada tu kitu ambacho kanisa lilikukwa linapinga.

Padre Valentine ambaye alikuwa Roma akawa anawahimiza vijana kufunga ndoa badala ya kufanya ngono bila ndoa kwani ni dhambi na kitu kisichokubalika mbele ya Mungu. Akawa anafungisha ndoa kwa siri kwenye makatakombe (mahandaki chini ya kanisa ambako kuna sehemu za ibada kwa watu wachache), alifanya hivyo kwa vile kufunga ndoa hadharani ilikuwa ni kukiuka amri ya wakuu wa dola ya kirumi.

Baadhi ya watu walifichua siri hiyo, hivyo Padre Valentin alishikwa na dola ya Warumi na kuuawa kama shahidi mfia dini kwa ajili ya kutetea waamini wake wafunge ndoa badala ya maisha ya ngono zembe bila ndoa.

Wakristo wakawa siku ya kumkumbuka Padre Valentin kama mfia dini sababu ya kutetea maisha ya wanakanisa kuwa wanandoa. Ikaenea katika kanisa nchi za magharibi na hata duniani ambako wanakanisa wanamkumbuka Mt. Padre Valentin. Baadaye ikapokeleka na watu hata wasio na imani ya kikristo kama ni siku ya kufanya kumbukumbu kwa Mt. Valentin kama mteteze wa Ndoa.

Maudhui ya siku hiyo kwa wasiowanakanisa imechukua maana nyingine ya kwamba ni siku ya wapendanao hata kwa wasio wanandoa bali mradi wanapendana, kitu ambacho ni kinyume cha malengo ya mfia dini Mt. Padre Valentin aliyetaka vijana wafunge ndoa badala ya kuwa na hawara tu (vimada).

AU WENGINE WANAISHUKULIA HIVI:

Asili yake ni sherehe ya kipagani iliyoanzia mjini Rome Italy.Ikaingia kuwa ya kidini na sasa imekuwa ikitumika kama ni msimu wa kufanya biashara huria ambapo biashara za vyakula na mapambo ya maua, dhahabu na vyakula kama chakleti huchangamka sana.

Warumi wa kale walisherehekea siku za tarehe 13,14 na 15 kwa matambiko mbali mbali yenye lengo la kutafuta uzazi kwa jina la siku ya Lupercalia.Wanyama wa kila aina walichinjwa ambapo vijana wa kiume walijitapakaza damu zao na kubeba mikia ya wanyama hao huku wakiwa uchi na kufukuzana na wasichana huku wakiwapiga migongoni kwa lengo na kukuza urutuba wa uzazi.Warumi hao waliamini kuwa muasisi wa mji wa Rome anayeitwa Romulus siku moja alinyonyeshwa na mbwa mwitu na ndipo akawa mwenye hekima na shujaa.

Ukristo ulipoingia Rome pole pole sherehe hizi ziliingia ndani ya mafundisho ya dini.Kwa mfano yapo masimulizi kwamba Valentine alikuwa ni kasisi (bishop) mnamo mwaka 197 A.D wa mji wa Interamna ujulikanao sasa kama Terni.Kasisi huyo aliuliwa na viongozi wa kijamii baada muda mfupi kutokana na imani yake ya kikristo.Inaaminika alikufa siku ya Februari 14.

Kisa kingine kinamtaja kasisi mwengine wa mji wa Rome kwa jina la Valentine ambaye naye inaaminika aliuwawa Februari 14.Kosa lake la mwanzo linatajwa kwamba akiwa jela aliweza kumponya upofu motto wa afisa gereza ambaye baadaye akafanya mahusiano naye ya kimapenzi.Alikuwa akiandikiana barua naye kwa kutumia damu yake kama wino.Hiyo barua ikiweka saini yake kama “From your Valentine”.Kisa kingine cha kufungwa kwake inasemekana mtawala wa Rome wa wakati huo Claudius alikuwa amekataza wavulana kuoa ili awe na askari wazuri.Kasisi Valentine aligundulika kufungisha ndoa kwa siri ikabidi akamatwe.

Mnamo mwaka 496 A.D papa wa wakati huo Gelasius kwa kuvutiwa na wimbi la sherehe za siku ya Valentine akaamua kwamba kila Februari 14 iwe ni siku ya sherehe ya kikristo kwa ajili ya kumuadhimisha St.Valentine.

Kuifanya Februari 14 kama siku ya wapendanao kulipata nguvu zaidi mwaka 1382 wakati Richard ? wa London alipotangaza uchumba na Anne wa Bohemia.Richard aliandika “For this was on St. Valentine's Day/ When every fowl cometh there to choose his mate.”.

Mwaka 1400 A.D mahakama maalum ilifunguliwa siku ya Valentine kushughulika na kesi mbali za mambo ya mapenzi kuhusiana na wachumba kupigana,kuachana na mateso mengine ya kimapenzi.

Kufikia mwaka 1601 sherehe za Valentine zilikuwa zimezoeleka sana katika maisha ya kawaida kiasi kwamba William Shakespeare aliandika katika shairi lake

“To-morrow is Saint Valentine's day,/All in the morning betime,/And I a maid at your window,/To be your Valentine.”.

Utaratibu wa kutumiana kadi za mapenzi ulianza rasmi mwaka 1847 jijini London wakati shughuli za uchapishaji ziliporahisika.Mwaka 1929 kwa mara nyengine sherehe za Valentine zilileta janga kubwa pale magenge matano jijini Chicago,Marekani yalipopigana na kuuana kwa risasi kuhusiana na mambo ya mapenzi.

Katikati ya ya miaka ya 1980 makampuni ya madini na biashara nyenginezo yalianza kuziteka nyara sherehe za Valentine kwa kuhamasisha watu kununua bidhaa zao.

Post a Comment

0 Comments