Header Ads Widget

Responsive Advertisement

BARUA YA MTOTO KWA MAMA YAKE



BARUA YA MTOTO KWA MAMA YAKE
*******:**;********
Mpendwa Mama.
Roho inaniuma, siamini kilichotokea. Nipo mbinguni sasa. Nilihitaji sana kuwa mtoto wako. Sijui nini kilichotokea nilipatwa na mshangao jinsi nilivyokuwa nikianza kukua. Nilikuwa katika giza lakini sehemu ambayo ni tulivu eti nimeambiwa ilikuwa ni sehemu inayoitwa mfuko wa uzazi.
Nilijiona nikianza kukua vidole vya mikono na miguu. Sikuwa mbali na kukua kabisa kuwa mtoto kamili. Nilitumia muda mwingi kulala na kufikiri jinsi maisha yangu yatakavyokua baada ya wewe kunizaa.
Hata hivyo siku za mwanzo kabisa nilijihisi na furaha sana kuwa sehemu ya nyama zako za mwili.
Wakati nimo tumboni mwako nilikusikia mara kadhaa ukilia nataka ujue tu kuwa ulivokua ukilia na mimi nilikuwa nalia vile vile, muda mwingine nilikusikia ukilalamika kabla ya kuanza kulia sio siri nilikuwa nikikuonea huruma sana mama. Nilimsikia baba akikufukuza na kunikataa nilishangaa kwanini ulikuwa ukilia sana. Kuna siku ulilia siku nzima, niliumia sana siku ile. Sikujua kwanin hukuwa na furaha.
Siku hiyo hiyo, kitu kibaya kilitokea. Kitu kama jinamizi kilikuja sehemu ambamo nipo ndani ya tumbo lako, nilikuwa nimetulia siku hiyo nikitafakari. Nilipatwa na hofu kubwa sana. Nilianza kulia, lakini hukunisaidia. Labda hukunisikia. Jinamizi lilizidi kunikaribia na nilizidi kulia mama!! Mama!! Mama!! Nisaidieeee lakini hukunisikia.
Nililia! Nililia! Nililia! Mpaka nilipojihisi siwezi kulia tena. Jinamizi likaanza kukata mikono yangu. Nilipatwa na maumivu makali ambayo siwezi kuyaelezea mama!
Nililia na kuomba jinamizi liniachie lakini halikuniacha, ndio kwanza likaanza kunikata miguu. Nililia sana lakini haukunisaidia wakati nilikuwa ndani ya tumbo lako.
Japo nilikuwa katika maumivu makali. Nilikuwa nakufa! Nilijua kuwa sitaweza kuiona sura yako tena wala kukusikia ukinibembeleza na kuniambia kuwa unanipenda!
Nilikuwa na mipango mingi kama ungenizaa, nilikuwa na mipango ya kukufuta machozi yako yote ambayo umekua ukikia mara kwa mara. Nilikuwa na mipango ya kukufanya uwe mwanamke na mama nwenye furaha. Sasa siwezi kutimiza mipango hiyo! UMENIUA MAMA! HUKUNIPENDA KAMA MIMI NILIVYOKUPENDA!.
Mbali na vyote nilihitaji sana kuwa mtoto wako. Nimekufa kifo cha maumivu mno, sijui walikufanya nini mama mpaka ukawa katili vile, ila japo nilikuwa na maumivu makali nilitaka nikumbie kuwa nakupenda mama kabla sijafa ila nilishindwa n namna gani nikufikishie ujumbe huo unielewe.
Na mwishoe sikuwa na pumzi tena za kukwambia chochote. NILIKUFA! Nilijihisi nikinyanyuliwa juu. Nilibebwa na malaika na kupelekwa katika sehemu ambayo ni nzuri sana. Nilikuwa bado nikilia. Lakini maumivu ya mwili yalikuwa yamekwisha.
Baada ya hapo nilikuwa na furaha tena! Nilimuuliza malaika ni nini kilichoniua. Alinijibu kuwa ni "MTOA MIMBA" mimi sijui Mtoa Mimba ni nini, ila labda ndio jina la yule jinamizi aliyenitesa ndani ya tumbo lako na kuniua.
Nimeandika barua hii kukwambia kuwa nakupenda mama na kukueleza ni jinsi gani nilitamani niwe mtoto wako. Nilijitahidi kweli Niishi. Nilitaka nami niishi niione Dunia ya mwenyezi Mungu, lakini nilishindwa Mtoa Mimba alikuwa na nguvu kunizidi mimi, alinivunja vunja mikono na miguu na kunitoa kwa nguvu tumboni kwako bila huruma wala ridhaa yangu.
Ilikuwa ni vigumu sana kuishi, nataka ujuwe kuwa nilitaka sana kuishi na wewe mama! Sikutaka nife! Na pia mama nakukumbusha sana kuwa makini na huyo mtoa mimba ni muuaji mkubwa, anaweza kuja kukuua na wewe au akaharibu tumbo lako wadogo zangu wasiweze kuja kukaa humo!
Nakupenda sana mama, na tambua kuwa nachukia kama na wewe utakuja kupata maumivu niliyoyapitia mimi kabla sijafa!
Tafadhali mama uwe makini.
Nakupenda.
Ni mimi mwanao.
"Nakuomba Nelea usitoe mimba yangu, Mungu akileta mtoto analeta na sahani yake"

PATA NAMBA YAKO YA KITAMBULISHO KWA KUPAKUA APP HII BOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments