Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Maajabu ya khanga!

Hakuna mwanamke ambaye hajawahi kuvaa khanga, vilevile hakuna mwanaume ambaye hajawahi kufunikwa na khanga (utotoni si ulibebwa )....Yafuatayo ni maajabu ya khanga

1/Historia
Asili ya vazi hili ni pwani ya Afrika Mashariki kama sehemu za Mombasa nchini Kenya na visiwani Zanziba. Ndio walikuwa watu wa kwanza kulivaa vazi hili na kuliheshimu.Haijajulikana ilikuwa ni miaka gani. Kwahiyo historia inaonyesha vazi la khanga limeasisiwa na watu wa pwani ya Afrika Mashariki

2/Fahari ya Mwafrika
Khanga ni fahari kwa wanawake wa kiafrika , Ni vazi ambalo limetumiwa miaka kwa miaka, kizazi kwa kizazi.....ni utambulisho wa waafrika na halichuji !!

3/Linapendwa na rika zote
Khanga ndio vazi linalopendwa na wanawake wa aina zote, vijana kwa wazee, mjini kwa vijijini ....ni mwendo wa kutupia khanga !!

4/Matumizi kibao
Khanga ni vazi lenye matumizi mengi pengine kuliko yote, linatumika kubebea watoto, kufungia ngata,kama kamba.taulo n.k

5/Khanga moko ni shida
Wanawake wakitupia khanga moko mwanaume lazima utoe jicho , khanga moko uswahilini ni balaa hadi kwenye vigodoro....mwanamke khanga!!!

6/Vazi linalosema
Khanga huwakilisha hisia za mvaaji kupitia maneno yaliyoandikwa, kuna vijembe, busara,matusi, hekima

Post a Comment

0 Comments