Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Kupunguza kuzeeka na kuwa na ngozi laini na changa

JINSI YA KUIFANYA NGOZI YAKO KUWA CHANGA NA KUPUNGUZA KUZEEKA

KUZEEKA KWA NGOZI NA JINSI YA KUPUNGUZA KUZEEKA
Kuzeeka ni utaratibu wa kawaida kwa mwili wa binadamu. Na hutokea kila siku kwa yeyote ambaye ameshafika umri wa utu uzima. Hakuna shida yoyote kwa mtu kuwa mzee isipokuwa kama mtu anapenda au anahitaji muonekano wa ujana – ngozi laini, nywele nyeusi nk

JINSI KUZEEKA KWA NGOZI KUNAVYOTOKEA
Kuzeeka kunatokana na kuharibika na kupungua kwa protini za ngozi zinazofanya kazi ya kuifanya ngozi iweze kukua, kuvutika na kutunza maji ya kutosha. Protini hizi huitwa elastin na collagen.
Protini hizo zikiharibika na kupungua ngozi hushindwa kukua, hushindwa kuvutika na hupoteza maji na matokeo yake huanza kufubaa, kuwa ngumu na kuwa makunyanzi.
Pia kushindwa kuvutika kwa ngozi ndio sababu ya mtu kuwa na michirizi.

JINSI YA KUPUNGUZA AU KUONDOA KUZEEKA KWA NGOZI
Kuzeeka kwa ngozi kunaweza kupunguzwa au kuondolewa kwa kuongeza uzalishaji na kiasi cha protini aina za elastin na collagen
Hilo linaweza kufanikishwa kwa vipodozi vya aina mbalimbali katika mfumo wa lotion, cream, mafuta na kadhalika
Hizi zitasaidia kuifanya ngozi kuwa changa na ya kuvutia kwa kuisaidia kukua, kuvutika na kutunza maji ya kutosha.

VITU GANI UTUMIE KUFANIKISHA HILI
Kuna bidhaa za aina nyingi na za kampuni mbalimbali za kuweza kufanikisha zoezi hili. Mfano wa kwanza ni vipodozi vyenye Vitamin A au mazao yanayotokana na Vitamin A (Lazima upate ushauri wa kitaalam ndipo uanze kutumia na zikusaidie vizuri)
Pia kuna vipodozi vyenye Vitamin E. Hivi navyo husaidia sana kuifanya ngozi kuwa laini na ya kupendeza, na kupunguza kuzeeka kwa ngozi.
Kitu cha muhimu ni kusaidia kuondoa ngozi iliyozeeka, kuongeza uzalishaji wa elastin na collagen na kuongeza maji na utunzaji maji katika ngozi (Moisturizer husaidia kukamilisha zoezi la kuongeza maji katika ngozi. Chagua iliyo bora kabisa na utumie).
Pia kunaweza kuwa na tofauti ya mahitaji ya bidhaa kati ya mtu na mtu, kwa hiyo ni vyema kila mtu kushauriwa kutokana na ngozi yake na mahitaji yake.
EPUKA VIPODOZI VISIVYO SALAMA NA VILE VISIVYOFAA KWA NGOZI YAKO. VINAWEZA VIKAKUHARIBU ZAIDI.

Post a Comment

0 Comments