Header Ads Widget

Responsive Advertisement

MSIBA ULIVYOMUUMBUA SISTA DUU



SIMULIZI FUPI - MSIBA ULIVYOMUUMBUA SISTA DUU


Usingethubutu kumtongoza kirahisi rahisi kamahuna roho ngumu!! Alikuwa haoni hatari kukutukana hadharani na kukuandikia STATUS…. Kilichompa jeuri ni kwamba alikuwa anakubalika sana. Akiweka status wanaume wanaishobokea sana wanamsifia.

Lakini bila kificho alikuwa ni mrembo sana!! Sio kwenye picha zake pekee bali hata waliopata bahati

ya kuonana naye ana kwa ana walikiri kuwa Neema alikuwa msichana mwenye mvuto wa pekee.. Alijua

kupangilia nguo na zikaifanya shepu yake ionekane vizuri. Alijua kutembea haswaa!!

Kubwa zaidi alikuwa anajua kutafuna wakati wa kula chakula, achana na wasichana wengi ambao ni

warembo na bado wakiwa wanatafuna chakula wanaacha midomo wazi. Neema alikuwa ana kitu

kingine cha ziada. Alikuwa anajua kutabasamu!!! Na kama angeamua kucheka basi alikuwa hachoshi

kumtazama. Nayasema yote haya kwa sababu na mimi nilipata

nafasi ya kuonana naye!! Kabla ya kuonana naye nilitumia zaidi ya akaunti

nne kumtongoza!! Nililazimika kutumia akaunt tatu tofauti kwa sababu Neema alikuwa ananiblock katika

account nyingine, Neema hataki maswali ya kijingajinga eti una miaka mingapi, sijui unaishi na

nani? Neema anapenda maongezi ya moja kwa moja we kama huna jipya basi achana naye. Ukimkosoa

katika Status yake anakublock, ukijishaua  kumwandikia ujinga kwenye WALL anakublock!!

Neema alikuwa Neema kweli. Akaunti ya kwanza nilijifanya mi najua kushauri,

alikuwa anatukanana na mtu nikamfuata inbox nikamwandikia, “Neema acha hizi mambo we kwa

urembo wako haupendezi ukitukana” baada ya  dakika tano nikaingia inbox. He! Nikashangaa

Neema ametoa picha ama? Maana hapakuwa na picha. Mbona jina la Neema limekuwa jeusi!!

Hapo ndipo nikapata fursa ya kuusoma ujumbe… “We mwehu nini, nenda ukamshauri baba yako

ajiunge facebook labda ndo anaweza kunishauri sio uchafu kama wewe” Wacha nipagawe!! Nikataka

kumjibu nikaambiwa haiwezekani. Neema alikuwa ameniblock!!!

Si unajua tena mwanaume hakubali kushindwa!! Nikaona nimedhalilishwa sana, nikafungua akaunti

nyingine, hapa sikuweka picha nikamuADD Neema akanikubalia, nikajiunga na Team ya kuLIKE, kila

annachoandika Neema mi naLIKE huku nikimsifia hata ujinga. Nikimfata inbox namsifia status zake

Hapa tukawa marafiki tena!! Si nikawa na haraka nikaanza kumtongoza Neema kitoto, eti ooh mara

nimwandikie usiku mwema baby!! Mara morning lovely one!!

Neema akashindwa kunivumilia akaniandikia bonge moja ya status…halafu akanitaja kabisa.

Ninachoshukuru sikuwa natumia jina langu halisi.


Baada ya hapo akaniblock. Sikukata tamaa

nikafungua akaunti ya tatu. Huku sasa sikuremba nikayafuatilia maisha ya Neema nikagundua kuwa ni

mtoto wa kidosi kwao kuna pesa. Nami nikaingia kipesa pesa. Post nyingi za Neema alikuwa

akiandika mara: “@Home sweet home watching movie!”

“@Samakisamaki” “Oh! At Maisha club jamani Diamond mchokozi

huyu!!” “Anyone around nipo kitanda cha sita kwa sita

alone!!” Nikagundua kuwa alikuwa mtoto wa kishua haswa!!!

Hatimaye nikafanikiwa kukutana na Neema kwa mara ya kwanza, Blue Pearl hotel Ubungo. Hapa

ndipo nikajua kwa nini Neema anaringa!! Alikuwa mrembo haswa na kama nilivyosema awali alikuwa

na vitu vingi ambavyo wasichana warembo hawana hasahasa jinsi ya kutembea maana warembo

wengine wanatembea kibabe kama wanyanyua nondo!! Neema alijua jinsi ya kuibana miguu yake

kisha ikaunda herufi kama V. mapaja yake manene yalikibeba kiuno chake vyema.

Baada ya kukutana ndipo nikaanza kuwa nawasiliana na Neema mara kwa mara. Japo

nilikuwa sijawahi kufika kwao lakini kwa mazungumzo yake nilifika kimawazo. Mara nipo na

fundi wa kutengeneza AC…..yaani msumbufu huyooo!!! Mara yupo na daktari wa mifugo ng’ombe

wao anaumwa Mara anaelekea airport kumpokea baba yake. Hapa nikamuuliza akaniambia baba yake

anafanya kazi uingereza. Nikamuuliza pia kuhusu mama yake akadai ana

saluni kubwa ka kike Kampala. Sasa hapa Neema akawa akiniomba hela ya vocha natuma elfu tano

hadi kumi. Tukitoka naye najiandaa na laki mbili na ziada!!!


IKAFIKIA SIKU YA SIKU!!

KWANZA nilishangaa kuna wadada wawili

walimuandikia Neema neno POLE katika WALL yake, lakini ghafla sikuona tena ile post na wala Neema

hakuwajibu!! Mchana tena kuna wavulana wawili wakamuandikia maneno ya kumpa pole. Uzuri

mmoja alikuwa rafiki yangu!! Nikamnukuu jina ‘CHIDY Boy Wa Mbinga!!!’ ile narefresh tu page

nikakuta Neema amefuta zile post!! Nikashangaa kulikoni!! Mara akaweka post kuwa ‘ambaye anajua jinsi ya kufunga WALL please anisaidie!!” baada ya dakika kumi WALL ya Neema ilikuwa imefungwa!!!

Nikajiuliza kulikoni!! Lakini sikumuuliza maana Neema hataki kuulizwa mambo yake ya facebook,

ukimuuliza anakwambia ‘sisi ni wapenzi tayari mambo ya facebook ya nini?’ ukiangalia kweli.

Unaacha!! Upesi nikamtumia meseji Chidy, nikamuuliza

unampa Neema pole kwa nini. CHIDY: ah amefiwa na baba yake bwana huyo

demu!!! MIMI: Baba yake? Lini. CHIDY: Jana usiku kaka kwani vipi?

MIMI: aah hamna kitu lakini vipi unamfahamu vizuri!!

CHIDY: hamna kaka simfahamu vizuri ila kifacebook tu!! Sema kuna watu wanasema anakaa

Mwananyamala kisiwani. Tukachat sana na Chidy hadi naye akaniambia kuwa

aliwahi kumtongoza na amemlia pesa zake kweli. Nami nikawa muwazi nikamueleza kuwa ni mpenzi

wangu japo sielewi kwanini ananificha kuhusu msiba. Mimi na Chidy tukakutana na kuamua

kufuatilia kwanini huyu Neema anaficha jambo la muhimu kama msiba. Safari yetu ikaishia

Mwananyamala Kisiwani. Tukaanza kuulizia wapi kuna msiba, kwa sababu

tuliamini kwa kuwa Neema ni mtoto wa kishua basi hata msiba ule utakuwa kama harusi kubwa!!! Mimi

nikiwa na lengo la kumfanyia surprise mpenzi wangu!! Baada ya kuulizia tukapata misiba miwili,

mmoja wa mtoto mdogo na mwingine wa Fundi viatu maarufu. Hapakuwa na msiba wa mtu kutoka

nje wala!! Mh!! Tukashangaa ina maana haijajulikana kama kuna msiba au??

Hapa sasa tukaamua kwenda kwenye huo msiba wa Fundi viatu, Chidy alishauri. Kweli tukafanikiwa

kufika, tukakuta watu wachache kiasi, Chidy alikuwa amechafuka na matope tayari kutokana na njia

mbaya tuliyopita. Si unajua tena uzuri wa surprise, hakikisha unayemsurprise hakuoni kabla wewe

hujamuona.


Sisi tukaanza kuuliza ni nani amefariki, tukaambiwa baba mwenye nyumba.

Mh! Chidy akaninong’oneza. “Hapawezi kuwa hapa kaka!!” nami nikakubali tena.

Tukauliza jina la marehemu, wakasema ni mzee Peter.

Akili ikakimbia upesi. Neema anajiita facebook “Ney Petersonn Daughter”

He!! Sasa inawezekana akawa ni baba yake Neema kweli ama!!

Wakati hu ulikuwa unapita mchango kwa ajili ya jeneza, hali ilikuwa tata na umasikini ulinukia eneo

lile. “Chidy eeh tubaki hapa hadi kieleweke!!”

Tukaamua kubaki!! Mara kwa mbali nikasikia mlio. “Chidy, simu ya Neema hiyo nilimnunulia inaita…

Chidy ni hapa.” Mara akatoka nje Neema ninayemfahamu, alikuwa peku na kanga imechakaa!!

Kichwani amejitanda kilemba. “We Chimodoi wewe!! Chimodoi nitakubamiza na hicho kisimu chako

nasema!!” mwanamke mmoja wa makamo alimkaripia Neema. “Mama si ninapokea mara

moja.” Akajibu Neema. Mama yangu weee!! Kumbe ndo kwao Neema hapa!! Sasa alikuwa anajikweza

nini maskini weee!! Sisi tukapiga picha kadhaa, nyumba na mazingira!!! Hatimaye mwili ulifika, kwa

ajili ya kuagwa!!! Hatujui nani alinunua jeneza!! Neema alipomaliza kuaga ndipo tukauvunja

ukimya..yaani kwa jinsi alivyotusumbua kumbe maisha duni kiasi hicho alaa!! Tukamfikia,

nikamgusa bega akageuka!! Aisee hadi leo sijui kama aidha aligongwa na gari huko alipokimbilia,

hatukjui kama labda alipatwa na uchizi kwa mshtuko ama vipi. Lakini alitimua mbio ambazo

sijapata kuona msichana akitimua!!! Aliteleza mara moja akaanguka akasimama kisha akatoweka hadi

leo ninapoandika simulizi hii…. Nilitamani sana kumkimbilia Neema lakini nikahofia kuandika hadithi

ndefu ikakuchosha kusoma ewe rafiki yangu!!!

SOMO:

Jikubali maisha yako yalivyo ndugu…kama

unalala chini sio lazima utwambie lakini basi usidanganye. Misiba inaumbua nyie, usidanganye

kwenu mambo safi kumbe kapuku sisi tukija msibani hatutaangalia kama upo katika machungu

tutakuuliza tu!!! Utuonyeshe yale magari sita, utuonyeshe ile bustani ambayo huwa unasema ni

kwenu, utuonyeshe na geto lako lenye kiyoyozi!!! Mnapiga picha nyumba za kulala wageni mnaandika

HOME SWEETv HOME....Shauri zenu!!

MWISHO!!!

Post a Comment

0 Comments